Natural Bliss

117. JINSI YA KUZUIA NYWELE KUKATIKA (NYWELE NATURAL/ZENYE DAWA (Relaxed)

 


Moja kati ya matatizo mengi ambayo yanawakumba watu wanaopenda nywele zao (hasa natural hair/nywele asili) ni kukatika (breakage).


🧚‍♂️Hapa tuelewane kitu kimoja, kwanza kuwa na nywele asili sio tatizo ila tatizo kubwa ni jinsi tunavyozitreat au kuzitunza nywele zetu.


🧚‍♂️Nywele huweza kukatika kwa sababu ya mambo ya hormone (kwa cases chache) lakini 90% inatokana na jinsi tunavyozihandle.

Inaweza kusababishwa na;

🌺Aina ya msuko unaosuka

🌺Aina ya bidhaa unazotumia kama zina viambata sumu

🌺Kitambaa unachofunga au kuvaa

🌺Hali ya hewa na aina ya maji ya sehemu husika

🌺Vitu unavyokula/Chakula

🌺Kutokunywa maji ya kutosha

🌺Kutumia moto mara kwa mara


Njia unazoweza kutumia ili kuzuia au kupunguza tatizo hili;

Kabla ya kutafuta njia ya kuondoa tatizo kwanza inatakiwa kutambua chanzo cha tatizo taratibu kama vile unavyotafuta chanzo cha allergy, mwishoni lazima utagundua chanzo cha nywele zako kukatika.

💐hakikisha nywele zako zina unyevu (well moisturised) wakati wote.

💐Zingatia aina ya misuko, nywele isivutwe sana na kupewa pressure kubwa (ngozi ya kichwa irelax)

💐Tumia LOC method kila unapoosha nywele zako.

💐Epuka kutumia moto mara kwa mara.


ITAENDELEA....

Post a Comment

0 Comments